MUHIMU KWA WALE WOTE WANAOHITAJI KUOMBA MIKOPO KUTOKA HESLB JUU YA UHAKIKI WA VYETI VYA KUZALIWA NA VIFO

Rita imetoa mwongozo ufutao;

Mwombaji anatakiwa kuwasilisha nakala ya cheti katika ofisi ya mkuu wa wilaya alikopata cheti cha kuzaliwa.

Waombaji wanaoishi nje ya WILAYA Waliopata CHETI cha kuzaliwa waingie katika mtandao kwa anuani:
http://uhakiki.rita.go.tz/uhakiki ili kupata maelezo ya jinsi ya kutuma nakala ya cheti na risiti ya malipo.

Baada ya uhakiki cheti kilichohakikiwa kitatumwa kupitia anuani ya mwombaji katika mtandao.

Ada ya uhakiki kwa kila cheti ni Tshs.3,000/=

ILIPWE KUPITIA BENKI YA NMB KWENYE AKAUNTI YA ADMINISTRATOR GENERAL COLLECTION ACCOUNT Na. 20610009881 au BENKI YA CRDB KWENYE AKAUNTI YA ADMINISTRATOR GENERAL COLLECTION ACCOUNT Na. 0150339892600
NOTE

kila mwombaji awasilishe/atume kivuli cha cheti kinachosomeka vizuri kwa ajili ya uhakiki ikiambatana na nakala ya risiti ya malipo.

Pia utaratibu uliotajwa hapo juu utatumika kwa ajili ya kuhakiki vyeti vya vifo vya wazazi.

Rita inapenda kuwasisitiza waombaji wote kufuata utaratibu ulioelekezwa hapo juu ili kuepuka usumbufu. Kwa maelezo zaidi piga simu namba *0800117482*

Imetolewa na wakala wa usajili na udhamini(RITA)
0 Comments